KWA NINI WANAUME WANAONGOZA KWA USALITI

UHUSIANO wa kimapenzi ni jambo gumu sana. Ugumu wake unatokana na ukweli kwamba, mwanaume aliyezaliwa na kulelewa katika mazingira tofauti, anakutana na mwanamke ambaye naye amezaliwa na kukulia katika mazingira mengine.

Wawili hawa wanaanza ukurasa mpya wa maisha, kila mmoja akiwa na historia tofauti kabisa ya huko alikotoka, unategemea itakuwa rahisi kwa wawili hawa kuishi bila misuguano?

Jibu ni HAPANA. Kwa lugha nyepesi, hakuna uhusiano wa kimapenzi ambao hauna changamoto na changamoto kubwa zaidi katika mapenzi ni usaliti.

Nimeshawahi kueleza huko nyuma na naendelea kueleza kwamba hakuna kitu kinachoumiza katika uhusiano wa kimapenzi, kama usaliti.

Ni ukweli kwamba licha ya usaliti kuwa jambo baya katika uhusiano, bado watu wanasalitiana kila kukicha.

Wanandoa wanasalitiana, wachumba wanasalitiana na hata wale ambao wapo kwenye hatua za awali kabisa kuelekea kwenye uchumba, nao wanasalitiana. Si ajabu hata wewe msomaji wangu, siku chache zilizopita umesaliti au umesalitiwa! Ni ukweli mchungu ambao ni lazima tujadiliane kuhusu namna ya kuukomesha.

Utafiti usio rasmi, unaonesha kwamba japokuwa wanawake na wanaume wote wanasaliti, lakini idadi ya wanaume wanaosaliti ni kubwa zaidi kuliko wanawake.

Kabla ya kujua sababu hizo, ni vizuri ieleweke kwamba katika kila usaliti unaotokea, kuna mambo mawili yaliyosababisha; matatizo katika uhusiano wa kimapenzi au matatizo ya mtu binafsi. Kama tunakubaliana katika hilo, hebu kila mmoja ajiulize, kwa nini wanaume wanaongoza kwa usaliti? Kwa nini wanaume wanawasaliti wake zao? Wanawake ambao wanafanya kila kitu kwa ajili yao?

TENDO LA NDOA Sababu kubwa inayofanya wanaume kuchepuka, ni kukidhi tamaa zao za kimwili. Utafiti uliofanywa na mtaalamu wa masuala ya kimapenzi, Dk Tamy Wilson wa nchini Marekani, unaonesha kwamba wanaume ambao wanatimiziwa haja zao za kimwili mara kwa mara bila vikwazo, wana nafasi ndogo ya kusaliti ukilinganisha na wale wanaopata haki ya ndoa kwa ‘mbinde’.

Kwa jinsi miili ya wanaume ilivyoumbwa, kadiri mtu anavyokaa muda mrefu bila kushiriki tendo, ndivyo tamaa za kimwili zinavyoongezeka na kama akishindwa kuwa makini, anaweza hata kutembea na hausigeli wakati ndani anaishi na mke mrembo mwenye sifa zote.

TABIA MBAYA Ukiachana na wale ambao wanasaliti kwa sababu hawana jinsi, lipo kundi lingine la wanaume ambao kihulka wana tabia mbaya tu! Atapewa kila anachokihitaji kwa mkewe, atahudumiwa kimwili, kiakili na kihisia lakini kwa sababu ana tabia ya kupenda kudanganya, kufanya mambo kwa siri na kukosa uaminifu, atasaliti tu.

Watu wa namna hii wanakuwa na matatizo ya kisaikolojia na mara nyingi, huwa hawadumu katika uhusiano hata mwanamke awe mvumilivu kiasi gani.

KUKOSA KUJIAMINI Sababu nyingine inayofanya wanaume wawe na tabia ya kusaliti mara kwa mara, ni kukosa kujiamini. Anaishi na mke au mpenzi mwenye sifa zote nzuri lakini moyoni mwake hajiamini, anahisi ipo siku mwanamke atamkimbia na kwenda kwa wengine, kwa hiyo kukitokea ugomvi kidogo ndani, anakimbilia kutafuta mwanamke wa pembeni akijidanganya kwamba hata mkewe akimkimbia, atakuwepo wa kumfariji.

JE WAJUA UKIMFANYIA HAYA MPENZI WAKO HAWEZI KUKUSAHAU KAMWE

Habari yako ndugu msomaji? Natumaini u mzima na mwenye afya njema.

1. KILA siku usisahau kumsifia kwa kumwambia ni kiasi gani alivyo mzuri. Kumbuka kila msichana anapenda kusifiwa hivyo unapomuambia yeye ni mzuri anaona una mthamini kuliko msichana yeyote awaye.

2. Wakati wowote ukipata nafasi muandikie barua au msg kwenye simu mueleze hisia zako kiasi gani unampenda. Kumbuka wasichana hupenda kusikia zaidi kutoka kwa wapenzi wao ni kiasi gani wanapendwa. Haitakiwi iwe tu katika kipindi cha siku ya wapendanao ndio umuoneshe kuwa unampenda. Muoneshe msichana ni kiasi gani yeye ni muhimu sana kwako.

3. Busu la ghafla na kumshika mkono wakati mkitembea pamoja itamfanya yeye kujisikia raha zaidi. Na wakati mwingine msuprise kwa kumtembelea mara kwa mara hi humfanya akuone wewe ni mtu muhimu pale usipokuwa naye karibu na kumfanya kukuhitaji zaidi ukiwa naye mbali

4. Tambua mahitaji yake. Uwe msaada kwake kipindi ambacho mpenzi wako amekasirika kuwa pale kwa ajili yake na ukimpooza kwa sauti ya upole na mahaba. Utashangazwa sana na kiasi gani msaada huo umeleta mabadiliko kwake. Hakikisha unamsaidia katika shida zake hapa ndipo kuna tatizo kwa wavulana wengi. Mapenzi si pesa lakini kuna kipindi ambacho pesa huitajika kulinda penzi lako. Si msichana anapokuomba pesa ina maana ana nia ya kukuchuna au amekupendea pesa kuna shida nyingine inabidi akuombe wewe tena kwa kukupima kama utakuwa tayari kumsaidia.

5. Mchukue mpenzi wako out mara nyingine itamfanya ajisikie furaha sana kwa sababu wasichana hupenda enjoyment na boyfriend zao. Hii haitamfanya mpenzi wako tu kuwa na furaha bali itawafanya nyie kwa pamoja kujuana na kufahamiana zaidi.

6. Kuwa muwazi kwake usimfiche jambo linalokuhusu. Msichana hupenda kutoa ushauri kwa mtu ampendaye hivyo unapokuwa muwazi atajisikia kuthaminiwa nawe na kukuona umemuamini

7. Ukijiona upo busy sana usithubutu kuacha japo kumpigia simu mara mbili kwa siku hata kama ukishindwa kumpigia wakati upo ofisini darasani au kwingineko hakikisha unapopata nafasi japo ujumbe mfupi wa kumwambia unampenda.8. Mkumbatie mara kwa mara katika tukio la kumbatizi kuna jambo kubwa sana hutokea. Si kwake tu hata kwako mvulana. Hali ya joto lenu huwaweka pamoja kifikra hata pale msipokuwa pamoja.

9. Epuka maugomvi na hasira za mara kwa mara ukiwa nae. Mwanamke hupenda ustaarabu kwa mtu ambaye yupo serious naye hivyo ukionesha hasira kabla hata hujamtongoza unaweza ukamkosa msichana hivihivi wasichana huwaogopa wavulana wenye hasira na wagomvi kwa sababu hupenda kubembelezwa.

10. Mdekeze. Msichana anapenda kudeka anaenda kudeka sana na kubembelezwa sana hivyo mvulana ukidekewa usikasirike eti huyu msichana kazidi wewe ndio wakati wako wa kumuonesha msuchana wako unampenda mdekeze mpaka aone aibu kudeka siku nyingine. Wasichana wameumbwa kwa jili ya wavulana ndio maana hudeka hii ndiyo silaha pekee na ya mwisho kumpata msichana hata kamasi wako ni wa rafiki yako unaweza ukatumia silaha hii kumpora msichana huyo kwa mwenzio usipojua kudekeza utaachwa pia.

JINSI YA KUAMSHA MAHABA NA MAPENZI KATIKA MAHUSIANO

Hizi hapa njia za kuamsha na kudumisha uhusiano mzuri kati yako na mpenzi wako hasa baada ya kuwa mmeshazoeana sana na kuhisi kuchokana.

Dumisha faragha katika mahusiano yenu

Hakikisha kunakua na faragha katika mahusiano yako na mpenzi wako. Vile vile itahakikisha kuwa wewe na mpenzi wako mnakuwa na wakati wa kutosha kustarehe bila wasiwasi. Usiruhusu siri zako na mwanamke zitoke nje kati yenu.

Tenga muda wa kustarehe pamoja

Ili kudumisha mahusiano na mwanamke lazima kuwepo na mda wa kuwa pamoja na kufanya mambo yenu mnayoyataka kwa kuridhika bila kupungukiwa na muda. Kwa mfano ni muhimu kupumzika mapema kitandani ili kuhakikisha mnakuwa na wasaa wa kutosha wa kufanya mapenzi.

Ongeeni pamoja kwa uhuru kuhusu suala la tendo la ndoa

Ni muhimu kujadili na kukubaliana na mwanamke kuhusu swala la kufanya mapenzi. Ni vyema muongee kuhusu suala la mapenzi na jinsi ya kuwasha moto wa mapenzi baada ya kuchokana. Mwanamke anatakiwa apewe uhuru wa kusema kile anachokihitaji.

Pang

eni miadi ya usiku

Mwanamke huridhika zaidi katika mapenzi kwa kuandaliwa ipasavyo hii ikiwa ni pamoja na kuwa na utayari wa kufanya mapenzi. Hivyo ni vyema kupanga miadi ya usiku ili mwanamke awe tayari na ili kumridhisha mwanamke.

Badilisha mazingira

Njia nyingine ya kuamsha mapenzi ni kubadili mazingira ya kufanyia mapenzi. Kwa mfano mnaweza kuacha kitanda chenu cha nyumbani na kulala katika chumba cha hoteli iwapo uamuzi huo utaboresha mapenzi kati yenu.

MAMBO AMBAYO MWANAMKE HAWEZI KUYAWEKA WAZI KATIKA MAHUSIANO

Unapoanzisha mahusaino na mwanamke yeyote yule fahamu fika yapo baadhi yavitu hawezikukwambia na baadhi ya mambo hayo ni;
1. Idadi ya wapenzi wake wa zamani
Wanaume wengi hupenda kujua wao ni wangapi kuwa na mwanamke Fulani. Lakini mwanamke kamwe hawezi akakwambia wewe ni wa ngapi. Kumuuliza jambo hili kunamkera sana mwanamke na ndio maana mara nyingi hawezi akakwambia ukweli.
2. Anakulinganisha na mpenzi wa zamani
Mwanamke mara nyingi anakulinganisha na mpenzi wake wa zamani japokuwa hawezi kukwambia waziwazi. Wakati mwingine tabia hii huwafanya wanawake kuwatamani wapenzi wa zamani na hata kurudiana nao endapo watakosa mtu aliye bora kuliko mpenzi wake wa zamani.


3. Kasoro zako
Mwanamke kamwe hawezi kukwambia kasoro zako. Wanawake wanajua kumfichiaa mpenzi wao mambo wasiyotaka yajulikane kwa wengine na kwa mpenzi wake. Wanajua njia za kiujanja za kutumia ili kufichua siri zako zote. Mwanamke hawezi kukwambia kasoro zako kwa kuogopa kukuumiza.


4. Mapungufu yake
Mwanamke hawezi kukwambia mapungufu yake labda kwa kuhofia kushushwa thamani. Wanawake ni wasiri sana kwa mapungufu yao. Wanajua vyema hofu zinazomuandamana, vitu vinavyowakosesha usingizi na mambo yanayowalemea maishani japo sio rahisi kuonyesha. Kwa nje anaweza akaonekana yuko vizuri na hana tatizo kumbe ndani ana matatizo au mapungufu. Anaweza kufanya yote kufunika upungufu wake!


5. Huwa unampagawisha mpaka anakosa la kusema.
Hili halisemi kabisa mwanawake kwa sababu anaona haya kutumia maneno ya wazi kueleza raha unayompa. Maneno ya kuzuzua ni himaya ya wanaume, lakini wakati mwingine wapo wasioweza kuficha.

6. Haumridhishi katika tendo la ndoa.
Wanawake wengi hawapendi kusema kama hawaridhiki Kwenye tendo la ndoa. Wanawake wanahitaji kuandaliwa vilivyo kwa dakika 10, 20 ama nusu saa. Mara nyingine wanaume huwahi kabla mwanamke hajawa tayari na hivyo kushindwa kuridhika lakini hawezi kusema.

Wanaume kabla ya kuoa huangalia mwanamke mwenye sifa hizi

Wanaume wengi wanapofikia hatua ya kuoa si kwamba wanakurupuka tu na kuoa mwanamke yeyote mwenye sura nzuri, bali huchukua muda wao mwingi kuchunguza mambo mengi juu ya wake ambao wanadhani kwamba wanaweza kuwa pamoja kwa kipindi chote cha maisha.

Wanawake wengi wanajisahau na kudhani kwamba kitu kinachoweza kuwafanya wakapata wachumba ni uzuri hivyo kupoteza muda wao kujichubua na kujiremba ili wawavutie wanaume bila kujua kwamba kuolewa ni zaidi ya uzuri.

Hali sasa hivi imebadilika ni tofauti na kipindi cha nyuma ambapo ukiwa na sura nzuri na umbo la kuvutia basi una asilimia 100 za kuolewa.

Utafiti ambao nimeufanya unaonesha kwamba zaidi ya uzuri wa tabia na umbo, kuna kuna sifa nyingine za msingi ambazo mwanamke anatakiwa kuwa nazo ili aweze kuwa katika mazingira mazuri ya kupata mchumba wa kumuoa kiasi kwamba asipokuwa nazo ataishia kuchezewa tu lakini haitatokea mtu kumtakiwa kwamba anataka kumuoa.

1. Mwenye mapenzi ya kweli.
Lengo kubwa la mwanaume kuoa ni kutaka kupata mapenzi ya kweli kutoka kwa mwanamke na ikiwezekana waweze kupata watotoa ambapo watoto hao ndio furaha ya ndoa. Wapo wanawake wengine ambao wanonesha wazi kutokuwa na mapenzi ya kweli bali wanakuwa na mapenzi ya kuzuga. Wanachotaka wao aidha kupata umaarufu tu kwamba yuko na mtu fulani ama kuweza kupata pesa alizonazo mwanaume lakini sio kwamba ana mapenzi ya dhati kutoka moyoni mwake.

Mwanamke asiye na mapenzi ya dhati utamgundua tu, muda mwingiutamuona macho yake yako kwenye mfuko wa mwanaume. Akiona kwamba mfuko umetuna utaona anaonesha mapenzi ya hali ya juu lakini pindi hali inapokuwa kubwa mbaya kifedha mapenzi yanaanza kufifia.

Kwanini wanaume wanapenda wana wake wenye mapenzi ya dhati kutoka mioyoni mwao na si kutokana na fedha walizonazo? Hii inatokana na ukweli kwamba maisha siku zote yanabadilika, kama waswahili wanavyosema, kuna kupanda na kushuka.

Sio kwamba kila siku utakuwa na maisha mazuri na kama itatokea hivyo basi ushukuru mungu.Hivyo basi mwanamke wa kuoa lazima afahamu hivyo na awe tayari kuonesha mapenzi yake ya dhati wakati wote wa maisha yao na si kwa kipindi fulani tu cha neema.

Si hivyo tu pia asilimia kubwa ya maisha ya ndoa yanatawaliwa na mapenzi, kwa hiyo nyanja hiyo inakuwa ya msingi sana kwa wanaume wengi kuiangalia ili wasije wakajikuta wanaoa mwanamke ambaye baada ya muda mapenzi yanakwenda likizo hali ambayo inaweza kuwafanya wasiishi maisha ya raha mustarehe.

2. Wenye tabia nzuri
Tabia njema ndio silaha ya maisha, ukiwa na tabia nzuri kila mtu atakupenda, hiyo ni katika maisha ya kawaida. Lakini linapokuja sualana kuoa tabia inakuwa kitu cha awali sana kungaliwa na hiyo inaweza kuwa na ukweli kwa sababu wapo wasichana wazuri wenye mvuto wa aina yake na maumbile mazuri, lakini wanakosa wanaume wa kuwaoa, ukiuliza kwani utaambiwa anatabia mbaya.

Naweza kusema hilo ndilo limekuwa tatizo kubwa kwa baadhi ya wanawake kukosa wanaume wa kuwaona. Hakuna mwanaume hata mmoja kati ya wale ambao nimejaribu kuongea naye ambaye ameonesha kulidharau suala hilo la tabia.

Si hivyo tu wapo wanaume ambao wameingia kichwa kichwa na kuoa kwa kuangalia sura tu bila kujali tabia, matokeo yake baada ya siku chache yanatokea machafuko ya aina yake hali ambayo imepelekea kuvunjika kwa ndoa kutokana na tabia mbaya alizonazo mwanamke.

3. Mwenye uchu wa maendeleo
Hivi karibuni kumekuwepo na mabadiliko ya aina yake kwa wanaume, wengi sasa hivi hawapendi kabisa kuoa mwanamke ambaye hana kazi yaani ‘golikipa’. Kama atakuwa hana kazi basi awe na uchu wa maendeleo kwa kujituma kufanya kazi mbalimbali za kimaendeleo kama vile kilimo kwa wale walio vijijini na biashara ndogondogo kwa wale ambao wako mijijini na hata vijijini.

Ile dhana ya kusema mwanamke ni mama wa nyumbani wa kukaa na kujipodoa akimsubiria mwnaume arudi amstarehesha, sasa hivi imepitwa na wakati. Wanaume wengi wanapenda wanawake ambao ni wahangaikaji, wenye ndoto za maendeleo katika maisha yao. Hata kama watakuwa si wafanyakazi lakini wawe wenye kutoa ushauri kwa waume zao juu ya jinsi gani wafanye ili wafanikiwe.

4. Wasiopenda makuu.
Kuna wanawake wengine wanakuwa na tabia za ajabu sana kiasi kwamba yaweza kuwa kero kwa wanaume. Wapo wanawake ambao wanapenda makuu bila kujali hali halisi ilivyo. Kuna wanawake naweza kusema wana tamaa, kila wikiendi utamsikia “leo tunakwenda wapi dear?”

Akimuona rafiki yake kanunua simuya laki tatu na yeye utamsikia akisema, ‘na mimi naomba uninunulie simu kama ya Grace’. Ukienda naye Pub anakuambia,”mimi sinywi pombe za chupa natumia za kopo tena Heineken’. Yeye hajali kiasi cha pesa mwanaume alicho nacho na usipotekelezea anachukia na anaweza hata kupunguza mapenzi.

Wanawake kama hawa wako katika mazingira magumu sana ya kuweza kupata wanaume wa kuwaoa. Mara nyingi katika maisha fedha huzungumza, kama mwanaume atakuwa na pesa ya kutosha itakuwa rahisi sana kwa mwanamke kupata kila atakachopenda lakini si kwa kumwambia mimi nataka kitu fulani.Mwanaune mwenyewe utamsikia akisema, ‘unataka nikununulie simu ya aina gani, au leo unataka twende wapi?’ hapo ndipo utakuwa na nafasi ya kusema, ‘mimi nataka uninunulie simu kama ya fulani ama leo nataka twende sehemu fulani.’

Wanaume ni warahisi sana wa kuwapatia wale ambao wanatarajia kuwaoa chochote ambacho watahitaji kama tu pesa haitakuwa tatizo. Kitu ambacho kinawaudhi wanaume wengi ni ile tabia ya mwanamke kupenda mambo makubwa bila kuangalia uwezo uliopo kwa mwanume.

Kuna wanawake wengine wao si wasemaji kabisa, yeye anasubiri leoamemletea hiki, anapokea na kushukuru, kesho akiambiwa twende beach anakubali. Au wengine wanasubiri mpaka waulizwe wanataka nini, ndio wanasema.

Sisemi kwamba uwe mkimya tu hata kama una shida ya kitu fulani na unafahamu kwamba ukimweleza mwenza wako anaweza kukusaidia, hapana! kama unaona kwamba uwezekano wa kupata kile ambacho unakihitajiupo mweleze kwa utaratibu naamini atakuelewa na kukutimizia.Tabia ambayo hawaipendi wanaume wengi ni ile ya kulazimisha ufanyiwe kitu fulaniwakati inawezekana uwezekano haupo.

5. Wavumilivu.
Wapo wanawake ambao sio wavumilivu kabisa katika maisha.Tunajua kwamba maisha siku zote hayatabiriki, yanaweza kutokea matatizo ya kiafya ama kifedha.Huu ndio wakati wa kuona uvumilivu wa mtu.Kama mwanamke anatarajia kwamba siku zote ni za raha tu na pindi matatizo yanapotokea anachukua uamuzi wa kumtoroka mwanume, huyo siyo mwanamke wa kuoa.

Wangapi leo hii huwatoroka waume zao pindi inapotokea kuumwa, kufilisika ama kupatwa na tatizo lolote ambalo kwa namna moja ama nyingine yanaweza kuwafanya maisha yao kutingishika?

Uvumilivu kwa mwanamke utakuwepo kama tu atakuwa na mapenzi ya dhati kama nilivyozungumza hapo awali. Mwanamke mweye mapenzi ya dhati ni lazima atakuwa mvumilivu na atakuwa tayari kuishi katika maisha ya aina yoyote, yawe ya raha ama ya starehe.Hawa ndio wale ambao wanaume wengi wengependa kuwa nao maishani mwao.

Kwa maana hiyo basi hiyo iwe changamoto kwa wanawake. Wajue kwamba wanaume wanafurahi kuwa na wanawake wa aina gani. Hata kama utakuwa umeshaolewa, kama kuna wakati kunakuwa na kutokuelewana baina yenu, chunguza yawezekana kwamba unakosa mojawapo ya tabia ambazo nimezitaja hapo juu. Waweza kubadilika kwani inawezekana.

Aina 10 ya wanawake wanaopendwa na wanaume

WENYE MSIMAMO
Wanawake daraja la kwanza wanaopendwa zaidi na wanaume ni wale wenye msimamo, uelewa mkubwa wa mambo na maamuzi sahihi, wako makini kwenye matendo yao na siku zote hufanya vitu kwa ajili ya kupata mafanikio.

WAPENDA USAWA
Aina ya pili inayohitajika katika katika ulimwengu wa kimapenzi ni wanawake wanaoheshimu usawa wa jinsia, walio tayari kubeba majukumu ya kifamilia kwa ulinganifu sawa na wanaume, wenye uwezo wa kuongoza jamii kwa asilimia 50 kwa 50.

WANAOJUA MAPENZI
Wanawake wajuzi wa mambo ya faragha wanapendwa sana. Sifa yao kubwa ni uwezo wa kutosheleza katika tendo la ndoa. Tafiti zinaonyesha kuwa wanaume hupenda sana wanawake watundu katika mchezo wa sita kwa sita. Mara nyingi wanatajwa kuwa na uwezo wa kuteka akili za wanaume bila kujali sifa zao za nje au za ndani.

MARAFIKI
Wanawake wenye sifa sawa na rafiki ni aina ya nne inayowavutia wanaume. Wao hutegemea zaidi nguvu ya kushawishi inayotokana na namna wanavyojali na kujitolea kuhakikisha wanakuwa marafiki wa kweli kwenye shida na raha kwa wapenzi wao. Si wakorofi, waungwana na wapenda amani.

WA WAZI
Aina nyingine ya wanawake inayowavutia wanaume ni wenye msimamo na uwazi. Si wepesi wa kuburuzwa katika maamuzi ya msingi kwa kisingizio cha wao ni wanawake. Utafiti unaonesha wanawake wa aina hii wamekuwa muhimu hasa kwa wanaume wenye tabia za ubabe na udhaifu katika uelewa wa mambo.

WANAOJITEGEMEA 
Wanawake wanaojitegemea wana soko kubwa kwa wanaume tofauti na akina naomba vocha kila siku. Uchunguzi unaonyesha kuwa wanaume wa leo hawapendi wanawake tegemezi, wasiokuwa na kazi na wanaoendekeza starehe za upande mmoja.

WASIO NA PRESHA
Nikisema wanawake wasiokuwa na presha namaanisha wasiolazimisha vitu vitokee haraka haraka. Wao siku zote huacha mambo yatokee yenyewe na kazi yao kuwa ni kutenda sehemu ya majukumu yao kama wapenzi.

MARIDADI 
Kundi lingine la wanawake wanaopendwa na wanaume ni wanaozingatia usafi na kujiremba. Wanaokwenda na wakati katika mavazi na mvuto wa nje. Lakini pia ni welewa wa mazingira, si wasamba. Wanapendeza kwa muonekano.

WANAORIDHIKA
Wanawake ambao hulidhika na hali walizonazo ni kivutio kikubwa kwa wanaume, hili ni kundi linalohitajika sana katika ulimwengu wa mapenzi kwa upande wa wanaume ambao maisha ya sasa yamekuwa yakiwageuza kutoka juu kwenda chini au chini juu. Kukubali hali zote bila kubadili tabia ni sifa njema ya mwanamke.

WA MMOJA
Wanawake wanaochagua mara moja na kutosheka na kuwa tayari kukwepa kila aina ya vishawishi toka kwa wanaume ambao kimtazamo wana vitu vya ziada zaidi ya waliowachagua mwanzo wanahitajika sana. “Niliye naye ananitosheleza kwa kila kitu sitaki mtu mwingine.” Kundi la wanawake wa aina hii ni adimu na muhimu sana.

Jinsi ya kuamsha mahaba na mapenzi katika mahusiano

Hizi hapa njia za kuamsha na kudumisha uhusiano mzuri kati yako na mpenzi wako hasa baada ya kuwa mmeshazoeana sana na kuhisi kuchokana.
Dumisha faragha katika mahusiano yenu
Hakikisha kunakua na faragha katika mahusiano yako na mpenzi wako. Vile vile itahakikisha kuwa wewe na mpenzi wako mnakuwa na wakati wa kutosha kustarehe bila wasiwasi. Usiruhusu siri zako na mwanamke zitoke nje kati yenu.

Tenga muda wa kustarehe pamoja
Ili kudumisha mahusiano na mwanamke lazima kuwepo na mda wa kuwa pamoja na kufanya mambo yenu mnayoyataka kwa kuridhika bila kupungukiwa na muda. Kwa mfano ni muhimu kupumzika mapema kitandani ili kuhakikisha mnakuwa na wasaa wa kutosha wa kufanya mapenzi.
Ongeeni pamoja kwa uhuru kuhusu suala la tendo la ndoa
Ni muhimu kujadili na kukubaliana na mwanamke kuhusu swala la kufanya mapenzi. Ni vyema muongee kuhusu suala la mapenzi na jinsi ya kuwasha moto wa mapenzi baada ya kuchokana. Mwanamke anatakiwa apewe uhuru wa kusema kile anachokihitaji.
Pangeni miadi ya usiku
Mwanamke huridhika zaidi katika mapenzi kwa kuandaliwa ipasavyo hii ikiwa ni pamoja na kuwa na utayari wa kufanya mapenzi. Hivyo ni vyema kupanga miadi ya usiku ili mwanamke awe tayari na ili kumridhisha mwanamke.

Badilisha mazingira
Njia nyingine ya kuamsha mapenzi ni kubadili mazingira ya kufanyia mapenzi. Kwa mfano mnaweza kuacha kitanda chenu cha nyumbani na kulala katika chumba cha hoteli iwapo uamuzi huo utaboresha mapenzi kati yenu

Jinsi ya kutumia sekunde tatu kumtongoza mwanamke

Habari za muda huu mdau na mfuatiliaji wa makala mbalimbali zinazokujia kupitia mtandao huu wa Muungwana Blog bila shaka umzima wa afya na unaendelea vyema na majukumu yako ya kila siku.

Naomba nichukue walau dakika zako chache kuweza kukujuza mbinu hii ya sekunde tatu kuweza kumtongoza mwanamke yule umtakaye na endapo utatumia sekendu hii tatu mwanamke huyo ni lazima atakuwa wako.

Sekunde tatu ni sekunde za maangamzi dhidi yako na yule unayemuona mbele yako. Endapo ukimwona mwanamke ambaye unataka kumtongoza, kwa kawaida kuna zile sekunde tatu za kwanza ambapo unafaa uchukue hatua kabla ile sauti ambayo inajaribu kuongea na wewe kukuzuia kufanya hivyo.

Tunasisitiza uchukue hatua ya kuweza kumtongoza mwanamke huyo ndani ya sekunde tatu kwani ukishindwa kufanya hivyo basi mwanamke huyo atapita bila ya wewe kuweza kufanya hivyo.

Kila mwanaume akichelewa kuapproach mwanamke kuna ile sauti ambayo inaanza kukuongelesha kwamba sijui hamna kitu hapo, hii ndiyo ile sauti ambayo inawafanya wanaume wengi wabaki kuwa single milele.

kwahiyo la kufanya hapa ukimwona mwanamke unayetaka kumuapproach basi fanya fasta. Una sekunde tatu za kuweza kufanikisha mpango mzima la sivyo kila msichana mzuri anayepita mbele ya macho yako utaendelea kumuita shemaji.

Jinsi Ya Kumzuzua Mwanamke Na Kumsuka Mpaka Akupende

Kila mwanaume anapenda kutaka kujua jinsi ya kumzuzua mwanamke mpaka ampende. Lakini wengi hushindwa kutimiza azma hii kwa kuwa hawajui mambo muhimu ya kufanya ili aweze kumzuzua mwanamke.

Je, uko tayari kuzijua mbinu TANO kuu za kumfanya mwanamke azuzulike kwako?

Najua labda ushawahi kuwaona mwanamke fulani wakiweza kuzuzuliwa na mwanaume, na mwanamke kama huyu anacheka mara kwa mara huku akikiri kuwa mwanaume flani anajua kuzuzua. Well, waonaje kama ni wewe sasa hivi unapewa sifa kama hii?

Kupewa sifa ya kuwa mzuzuaji na mwanamke ni sifa kubwa zaidi kwa mwanaume kutoka kwa mwanamke. Na si kwa ajili ya sura, shepu wala ujanja wako. Yote itategemea na kipawa chako na tajriba yako wa kuzuzua.

So, utamzuzua vipi mwanamke?

Kumzuzua mwanamke kutategemea uwezo wako wa kuwasiliana na yeye na kumfanya ajihisi kuwa na furaha wakati wote. Tumia mbinu tano ambazo tumezihakikisha utendaji wake.

#1 Ongea na yeye mambo ambayo anataka
Unaweza kuona kuwa haina umuhimu wowote, sababu wanaume wengi hufanya hivi. Wanaume wengi hubaki wakijiuliza kuna haja gani  kwao kuongea mambo ambayo mwanamke anataka kuongea. Mbona wanawake hawawezi kuongea mambo ambayo mwanaume pia anataka?

Bila shaka, wanawake wanaweza. Wanawake pia wanakuwa active kutaka kujua aina ya mwanaume ambao wanajihusisha nao. Lakini wakati mwingine, haswa unapotaka kumfurahisha na kuteka atenshen yake kwako, ni vizuri kujua mambo ambayo yanagonga ndani ya kichwa cha mwanamke. Na kumakinika kuteka atenshen yake haimaanishi kuwa mwanaume anapaswa kuongea kuhusu mambo ya vipodozi na urembo na mwanamke, La. Daraja kati ya mwanaume na mwanamke imepungua siku hizi. Ni rahisi kuongea na mwanamke mambo ambayo anapenda bila hata kutatizika. Bora tu uhakikishe kuwa utaweka kando maswala ya mipira, elekroniki na hesabu katika mazungumzo yenu.

#2 Msuke
Wakati unapozungumza na mwanamke, ni rahisi kumfanya aweze kuongea na wewe. Lakini hio haitoshi. Kama unataka kumzuzua mwanamke basi unahitajika kumfanya ajihisi huru, na pia umuonyeshe kuwa uko interested na yeye.

Marafiki hawawezi kuzuzuana hadi wavuane chupi. So kama utaongea na yeye kama rafiki yako basi atakuona tu kama mwanaume anayevutia. Lakini hatakuona kama mwanaume anayezuzua. Kutaka kuonekana kama mwanaume mweye uwezo wa kuzuzua machoni mwa mwanamke, basi unahitajika kumfanya akuone wewe kama mwanaume ambaye anaweza kutoka naye deti. Na kufanya hivyo lazima umsuke.

Na unapochukua hatua ya kumsuka hakikisha kuwa hautumii maneno kama ‘unapendeza’, ‘leo umerembeka’, ama kutumia mstari wowote ambao unaendana na hii. Inaboesha na haionekani kuwa na uhalisia wowote. Badala yake tumia maneno ambayo yanamlenga yeye moja kwa moja. Umemuona amepaka wanja kwa macho? Mwambie “Leo nauona utofauti kwa sura yako, kwani umejipaka nini?” akijibu hajui, ama akikwambia ni wanja mtamkie, “Basi unapendeza kupindukia, hata nashindwa kuacha kukuangalia.” Haya ni baadhi ya maneno ambayo unaweza kumsifia yeye binafsi na moja kwa moja.

Kwa kumsuka utakuwa umefanya mambo matatu wakati mmoja. Kwanza ni kuwa umemchangamsha kwa kumfanya atabasamu. Pili umemfanya atambue kuwa wewe umemuona anapendeza. Na tatu ni kuwa umemuonyesha kuwa umevutiwa na yeye. Yote haya ni ya kufanya ili akutizame kama mwanaume ambaye anaweza kutoka deti na yeye.

#3 Kuwa mcheshi
Kufikia sasa kwa kuwa tayari ushamfanya kuwa na tabasamu kwa kumsuka, ni wakati wa kuingia katika himaya yake binafsi. Kila mtu huwa na himaya yake binafsi na kawaida hatujihisi huru iwapo mtu mwingine ataingia katika himaya zetu unless mtu huyu ni mtu ambaye tunajihisi comfortable naye. Ok, kwa kueleza juu juu ni kuwa mfano hauwezi kumuaproach mwanamke usiyemjua halafu uende ukakae na yeye sako kwa bako na uongee na yeye kana kwamba ni mtu unayemjua na kufahamiana naye tangu kitambo bila kufuata taratibu zake.

Kumfanya ajihisi huru na wewe, lazima uwe na muda  mrefu na yeye ili akuzoee. Akikuzoea hapo sasa unaweza kutumia ucheshi ambao unaweza kuutumia kwa manufaa yako. (machapisho ya awali tuliongea kuhusu jinsi ya kuwa mcheshi)

Hapa hakikisha kuwa wakati unapomchekesha mwanamke usitumia wala usijilazimishe kutumia hekaya ama stori za kuchekesha ulizozisikia mahali ama kusoma kitabuni. Kinachohitajika kwako ni kuwa mhalisia tu, mwanamke akipendezwa atacheka tu.

#4 Mtongoze
Wanaume huwatongoza wanawake kila wakati, lakini wakati mwingine wanawake wanahisi kuwa wanaume wanaowatongoza ni mafala. So usivuke mipaka yako wakati unapomtongoza sababu anaweza kukubeza. Mbinu rahisi ya kuanza kutongoza ni kwa kuanza kwa wepesi. Muulize wikendi atakuwa wapi baada ya shughli zake za wiki, muulize kuhusiana na sehemu anayopenda kubarizi na pia mkahawaha anaoupenda, na kitu chochote kile kinaweza kuhusiana na yeye moja kwa moja. Atajua kuwa unajaribu kumtongoza kwa sababu hakuna mtu anaweza kuuliza maswali haya bila lengo madhumuni.

Halafu mrushie hili swali.

“Enhe, hii inaweza kuwa personal, hivi wewe una boyfriend? Kama uko naye, basi moyo wangu naona unaweza kuyayuka wakati wowote kuanzia sasa!”

Hii inaweza kuoneka nzito lakini hufanya kazi wakati wote.

Atacheka, lakini mstari huu utakuwa umepitisha lengo lako kwako, na atajua kuwa uko interested na yeye. Lakini usifanye mambo yaende segemnege kwa kunyamaza kwa muda baada ya kukupa jibu lake. Endelea na stori nyingine ujifanye kana kwamba swali hilo halikuwa na umuhimu wowote kwako. Lengo lako umeliweka wazi lakini hutaki ajihisi kuwa hayuko huru mbele yako.

#5 Mguse
Hii ni sehemu hatari, lakini unahitaji muda kujifundisha. Unataka kujua jinsi ya kumzuza mwanamke, sawa? Basi kumgusa wakati ufaao inakupa point tano muhimu ambazo unahitaji kujua ili umzuzue mwanamke. Kama umepata kila kitu sawa, basi utakuwa umefanikiwa kwa kila kitu.

Lakini tena kumgusa mwanamke ni sawa na kucheza na moto. Ukiwa na haraka ya kuuguza hautahisi lile joto. Na ukikaa muda mrefu ukiugusa, utachomeka. Unaona venye hatari iliopo hapa?

Unaweza kutuma msisimko hadi kwa uti wake wa mgongo kwa kumgusa kiulaini kama tayari umemchangamsha awali. Lakini kumbuka hili, mguse wakati ambao unataka kumgusa pekee, kama vile kugusa sikio lake wakati unapomsifia kuhusu vipuli alivyofaa, kupapasa nywele zake wakati kuna upepo mkali, ama kuuwekeza mkono wako nyuma yake wakati mnavuka barabara. Mguso ni njia ya kuingia katika hulka ya mwanamke, so unahitajika kuwa makini zaidi na umsome vile ambavyo atareact kabla umguse kwa mara ya pili.

Upo?

Hizi ndio dalili 8 za kuonyesha umependwa na mwanaume lakini anaogopa kukuambia.

Tukija maswala ya kutongoza, kuna mitindo tofauti tofauti ambayo wanaume hutumia ili kufaniikisha lengo lao. Kuna ule msemo unaosema ‘mwenda tezi na omo marejeo ni ngamani, yaani unaweza kufuata njia tofauti tofauti kufika pahali lakini mwishowe utarudi pale pale sehemu moja, kewahiyo  kwa wanaume kila mmoja ana mbinu yake ya kutongoza. Usije kusema kuwa mwanaume mwenye aibu hajui kutongoza akiwa na wewe, labda hio aibu yake ni moja ya mtego aliouweka spesheli wa kukunasa wewe.

Je utajuaje kama mwanaume mwenye aibu amekuzimia lakini hataki kuonyesha?

1. Anaingiwa na wasiwasi akiwa na wewe
Ukiona mwanaume anaingiwa na kibaridi ama kupapatika akiwa kando yako ujue ni ishara ya kukuambia kuwa amekuzimia. Hii inatokea wakati mko pamoja halafu anaingiwa na wasiwasi mara anafanya hivi mara vile.

2. Anapenda kuulizia marafiki zako kukuhusu
Mwanaume mwenye aibu akikupenda huwa anataka kukufahamu zaidi kukuhusu. Iwapo atashindwa kuongea na wewe moja kwa moja basi ataanza kuwaulizia marafiki zake kukuhusu. Ukiona mwanaume ana tabia kama hii ya kuulizia marafiki zako, lile la kufanya nikuonyesha ishara za kuwa uko huru kuongea nayeye wakati wowote ule anapojiskia huru.

3. Anakuwa na tabia isiyoeleweka akikuona
Wakati mwingine inatokea ya kuwa mwanaume mwenye aibu anashindwa kustahamili kuonyesha hisia zake hivyo kujaribu kuzificha ili usiweze kuzitambua. Lakini badala ya kuzificha, huibua tabia nyingine ambazo hazina mfanano wa kwake. Usishtuke ukiona akifanyika mambo ambayo si ya kawaida manake wewe ndio chanzo kikuu cha kufanyika hivyo. Yaani utakuwa umempagawisha kiasi cha kuwa anaweza kuanza kuchora miduara kwa mchanga akitumia miguu yake.

5. Anapenda kutabasamu na wewe
Wanaume wote kawaida wakipendezwa na mwanamke huwa wanatabasamu. Lakini kwa mwanaume mwenye aibu aliyekupenda huwa tabasamu lake ni tofauti. Mara nyingi atakuwa akitabasamu lakini mara kwa mara anashindwa kukuangalia usoni. Labda anaweza kukuangalia lakini pindi utakapomuangalia yeye atajifanya anaagalia kando. Hii ni baadhi ya tabia ya wanaume wa aibu hufanya wakati anapojaribu kukupendeza.

6. Anakuwa kimya ukiwa naye
Anaweza kuwa anaongea na marafiki zake sehemu flani, lakini pindi utakapotokea ananyamaza kabisa ama kuanza kuongea maneno yasiyoeleweka. Hata usishangae iwapo atakataa kujibu salam zako kama umempata katika hali kama hii. Mara nyingi ukimkuta akiwa na maongezi na marafiki zake, atajifanya hata hakuwa akizungumza katika kuchangia maongezi.

7. Anabadilisha mwonekano wake
Ukiona kuwa mwanaume mwenye aibu ameanza kubadilisha mionekano yake kwa kuanza kuvalia nguo tofauti, mitindo mipya ya nywele nk akiwa na wewe, jua hii ni ishara ya haraka kuonyesha kuwa amekuzimia.  Kufanya hivi kwa kawaida ana makusudio ya kukuridhisha wewe. Labda anadhania ya kuwa kuna mtindo fulani ambao akiuvaa unakupendeza.

8. Anagugumiza akiongea na wewe
Mwanaume huyu hujamsikia akikwamakwama wakati anapoongea lakini ghafla unamskia akigugumiza anapoongea na wewe. Hii ni ishara ya kuonyesha kuwa anaishiwa na maneno ya kukuambia na inakuwa vigumu kwake kuyatoa ama kutafuta maneno ya kukuambia.

Je ni kitu gani kinachowafanya wanaume aina hii kuwa spesho kwa mwanamke?
Kuna wanawake ambao wanapenda wanaume ambao ni wa aibu kwa kuwa hawana mambo mengi. Lakini usishangae kumwona mwanaume wa aina hii akikuapproach akutoe mkale bata pamoja. Pia aina hii ya wanaume itafikia wakati fulani wanaweza kukushangaza kwa kufunguka na kugundua kuwa ilikuwa tu ni baadhi ya mbinu waliyotumia kukuteka kimapenzi.

Design a site like this with WordPress.com
Get started